zanzibar hip hop

Promote your mixtape at ReverbNation.com

Artst & Presenter &Producers

Sunday, June 9, 2013

PICTURES 3 ZA HARUSI YA H.BABA NA FLORA MVUNGI




WAFAHAMU WASANII WALIOSHINDA TUZO ZA KILL MUSIC AWARDS 2013 ILIYOFANYIKA JUNE 8 PALE MLIMANI CITY

              Mrisho Mpoto akikabidhiwa tuzo ya wimbo bora wenye vionjo vya asili "Chocheeni kuni:"

               Ben Pol akiwa kwenye stage na tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Mashairi Bongo Fleva.


MASHUJAA BAND KALA JEREMIAH NA OMMY DIMPOZ WANG'ARA KTMA


Usiku wa jana ulikuwa ni usiku wa furaha sana kwa Mashujaa Band ambao waliongoza kwa kuondoka na tuzo nyingi kuliko wasanii wengne. Mashujaa ambao wanafanya vizuri na wimbo wao wa ''Kidole Risasi'' waliondoka na kura 5 ikiwa ni pamoja na msanii bora wa kiume band Charz Baba, mtunzi bora a mashari ya band Charz Baba, rapper bora wa band Furguson, wimbo bora wa band Risasi Kidole na tuzo ya tano waliichukuwa kupitia category ya band bora ya mwaka huku wakiwatupa kule Twanga Pepeta, Mapacha Watatu na Msondo Ngoma



EXCLUSIVE MSIKILIZE DIAMOND AKIELEZEA SABABU YA JANA KUTOHUDHURIA TUZO ZA KILIMANJARO

Hitmaker Diamond Platnumz jana hakuweza kuhudhuria tuzo za Kili licha ya kushinda tuzo mbili kubwa zilizopokelewa na watu wengine kwa niaba yake. Diamond amezungumza na Bongo5 kueleza sababu iliyomsababisha ashindwe kwenda kupokea tuzo zake mwenyewe. Amesema alishindwa kwenda kwenye kilele cha tuzo hizo kubwa nchini zilizotolewa jana kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam kwakuwa alitakiwa kwenda kwenye uzinduzi wa kinywaji kipya cha kampuni ni ya Cocacola, kiitwacho Novida uliofanyika jana usiku kwenye mgahawa wa Akemi uliopo kwenye jengo la Golden Jubelee, jijini Dar. Amesema akiwa kama balozi wa Cocacola ilikuwa ni lazima ahudhuria uzinduzi huo. Diamond alishinda tuzo mbili ikiwemo kubwa ya msanii bora wa kiume.Msikilize zaidi hapa ambapo anawashukuru pia waliompigia kura

Wednesday, June 5, 2013

HAKIKA NGWAIR ALIKUWA MTU WA WATU,HUU NDIYO UMATI ULIOJITOKEZA KUMUAGA

msiba_wa_mangweah_05062013_02
Hakika Ngwair alikuwa ni mtu wa watu,hawa wote
 waliacha shugri zao ili tu angalau wapate fulsa
 ya kuuona mwili wake kwa mara ya mwisho........

Tuesday, June 4, 2013

KAMPUNI YA KUUZA RINGTONES ZA KAZI ZA WASANII NA BONGO RECORDS ZATOA TAMKO JUU YA MAUZO YA KAZI ZA NGWEA

kumuenzi na kuenzi kazi zake ili ziendelee kuishi daima na familia na kazi zake.

yake iweze kufaidika Kampuni inayojishughulisha na mauzo ya ringtones za kazi za wasanii "Push Mobile" na studio iliyofanya kazi nyingi za msanii marehemu Albert Mangwea zimetoa tamko juu ya mauzo ya kazi za Mangwea, ambapo imeomba mashabiki wake wanunue kazi hizo kwa wingi kupitia mitandao ya simu kwa kupitia Code Maalumu, kama njia moja wapo ya kuenzi kazi zake

WAKATI WASANII WENZAKE WAPO WANAPOKEA MWILI WA MAREHEMU NGWAIR MSANII DIAMOND, ALIKUWA APONDA MARAHA BAHARI YA HINDI

diamond ali post Picha akiendesha boti la kifahari katika
bahari ya hindi jijini Dar es salaam na
rafiki zake.MASHABIKI WAMPONDA KATIKA

MTANDAO MARA BAADA YA
KUPOSTI PICHA ZA KUONYESHA YUPO BATANI

Maelfu wampokea Marehemu Ngwea











Mwili wa aliyekuwa msanii mahiri katika game ya Bongo Flava hapa Tanzania, Albert Mangwea umewasili leo nchini kutokea Afrika Kusini na kupokelewa na umati wa ndugu, marafiki na mashabiki wa kazi zake ambao kila mmoja ameguswa kwa namna yake na msiba huu mkubwa, Na hii ni tayari kwa shughuli za kutoa heshima za mwisho hapa jijini Dar siku ya kesho kabla ya kuelekea Morogoro kwaajili ya maziko.

Hali imekuwa ni ya hamaki na huzuni katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere wakati wa kuwasili kwa mwili huu ambapo hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa.

Wasanii mbalimbali wameweza kujitokeza ikiwepo kubeba msalaba na kusindikiza gari lililokuwa limebeba mwili wa marehemu na sehemu kubwa ya watu wakiwa wanataka jeneza lishushe kwenye gari na kubebwa na wao.

Raia hawa waliojitokeza kwa maelfu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kuonyesha ni kwa jinsi
gani walikuwa wakimpenda marehemu