CHIWILEINC
Sunday, June 9, 2013
WAFAHAMU WASANII WALIOSHINDA TUZO ZA KILL MUSIC AWARDS 2013 ILIYOFANYIKA JUNE 8 PALE MLIMANI CITY
Mrisho Mpoto akikabidhiwa tuzo ya wimbo bora wenye vionjo vya asili "Chocheeni kuni:"
Ben Pol akiwa kwenye stage na tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Mashairi Bongo Fleva.
Ben Pol akiwa kwenye stage na tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Mashairi Bongo Fleva.
MASHUJAA BAND KALA JEREMIAH NA OMMY DIMPOZ WANG'ARA KTMA
Usiku wa jana ulikuwa ni usiku wa furaha sana kwa Mashujaa Band ambao
waliongoza kwa kuondoka na tuzo nyingi kuliko wasanii wengne. Mashujaa
ambao wanafanya vizuri na wimbo wao wa ''Kidole Risasi'' waliondoka na
kura 5 ikiwa ni pamoja na msanii bora wa kiume band Charz Baba, mtunzi
bora a mashari ya band Charz Baba, rapper bora wa band Furguson, wimbo
bora wa band Risasi Kidole na tuzo ya tano waliichukuwa kupitia category
ya band bora ya mwaka huku wakiwatupa kule Twanga Pepeta, Mapacha
Watatu na Msondo Ngoma
EXCLUSIVE MSIKILIZE DIAMOND AKIELEZEA SABABU YA JANA KUTOHUDHURIA TUZO ZA KILIMANJARO
Hitmaker Diamond Platnumz jana hakuweza kuhudhuria tuzo za Kili licha ya
kushinda tuzo mbili kubwa zilizopokelewa na watu wengine kwa niaba
yake. Diamond amezungumza na Bongo5 kueleza sababu iliyomsababisha
ashindwe kwenda kupokea tuzo zake mwenyewe.
Amesema alishindwa kwenda kwenye kilele cha tuzo hizo kubwa nchini
zilizotolewa jana kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam
kwakuwa alitakiwa kwenda kwenye uzinduzi wa kinywaji kipya cha kampuni
ni ya Cocacola, kiitwacho Novida uliofanyika jana usiku kwenye mgahawa
wa Akemi uliopo kwenye jengo la Golden Jubelee, jijini Dar.
Amesema akiwa kama balozi wa Cocacola ilikuwa ni lazima ahudhuria
uzinduzi huo. Diamond alishinda tuzo mbili ikiwemo kubwa ya msanii bora
wa kiume.Msikilize zaidi hapa ambapo anawashukuru pia waliompigia kura
Thursday, June 6, 2013
Wednesday, June 5, 2013
Tuesday, June 4, 2013
KAMPUNI YA KUUZA RINGTONES ZA KAZI ZA WASANII NA BONGO RECORDS ZATOA TAMKO JUU YA MAUZO YA KAZI ZA NGWEA
kumuenzi
na kuenzi kazi zake ili ziendelee kuishi daima na familia na kazi zake.
yake iweze
kufaidika Kampuni inayojishughulisha na mauzo ya ringtones za kazi za wasanii
"Push Mobile" na studio iliyofanya kazi nyingi za msanii marehemu
Albert Mangwea zimetoa tamko juu ya mauzo ya kazi za Mangwea, ambapo imeomba
mashabiki wake wanunue kazi hizo kwa wingi kupitia mitandao ya simu kwa kupitia
Code Maalumu, kama njia moja wapo ya kuenzi kazi zake
WAKATI WASANII WENZAKE WAPO WANAPOKEA MWILI WA MAREHEMU NGWAIR MSANII DIAMOND, ALIKUWA APONDA MARAHA BAHARI YA HINDI
diamond ali post Picha
akiendesha boti la kifahari katika
bahari ya hindi jijini Dar es salaam na
rafiki zake.MASHABIKI WAMPONDA KATIKA
MTANDAO MARA BAADA YA
KUPOSTI PICHA ZA KUONYESHA YUPO BATANI
bahari ya hindi jijini Dar es salaam na
rafiki zake.MASHABIKI WAMPONDA KATIKA
MTANDAO MARA BAADA YA
KUPOSTI PICHA ZA KUONYESHA YUPO BATANI
Maelfu wampokea Marehemu Ngwea
Mwili wa aliyekuwa
msanii mahiri katika game ya Bongo Flava hapa Tanzania, Albert Mangwea
umewasili leo nchini kutokea Afrika Kusini na kupokelewa na umati wa ndugu,
marafiki na mashabiki wa kazi zake ambao kila mmoja ameguswa kwa namna yake na
msiba huu mkubwa, Na hii ni tayari kwa shughuli za kutoa heshima za mwisho hapa
jijini Dar siku ya kesho kabla ya kuelekea Morogoro kwaajili ya maziko.
Hali imekuwa ni ya
hamaki na huzuni katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage
Nyerere wakati wa kuwasili kwa mwili huu ambapo hii ndiyo hali halisi
ilivyokuwa.
Wasanii mbalimbali
wameweza kujitokeza ikiwepo kubeba msalaba na kusindikiza gari lililokuwa
limebeba mwili wa marehemu na sehemu kubwa ya watu wakiwa wanataka jeneza
lishushe kwenye gari na kubebwa na wao.
Raia hawa waliojitokeza
kwa maelfu walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za kuonyesha ni kwa jinsi
gani walikuwa wakimpenda
marehemu
Subscribe to:
Posts (Atom)


















