The Game anataka kuanzisha upya beef na 50 Cent?Ajiita ‘-Unit killer’


Rapper the Game ambae alizinguana na kundi la G-Unit na kuachana miaka mingi iliyopita amefunguka na kusema yeye ndiye muuaji wa kundi hilo linaloongozwa na 50 Cent.
Rapper huyo ambae hivi karibuni alitangaza kuwa amebatizwa na ameanza maisha mapya ya kiroho anaonekana kurudi nyuma kidogo na kuwachokoza G-Unit kundi ambalo members wake wa zamani wote waliondoka, Loyd Banks, Tony Yayo walifuata baada ya Game, lakini sasa 50 Cent amewasaini wasanii wapya ambao kiukweli hawana moto kama wale members wa zamani.
Game na 50 Cent waliingia katika mtafaruku mkubwa sana katikati ya miaka ya 2000 na Game akaanzisha kampeni inayoitwa G-U NOT. Na akasema kuwa 50 Cent aliandika wimbo wake ili aendelee kuwa juu kwenye kundi kwa kuwa alikuwa na ‘umimi’ na akaeleza kwa nini alikuwa na hasira dhidi ya 50 Cent na G-Unit. “300 Bars niliandika nikiwa na hasira sana na nilitaka G-Unit ife brand kama brand, recording label, ama group…kuna msitari niliandika ukisema you sell records but a G-G-G-Unot. Na baada ya hapo zikatoka T-Shirt na harakati zikapiga hatua hata zaidi yangu.”
Lakini mwezi march mwaka huu Game alipoulizwa kuhusu kilichotokea miaka hiyo kati yake na Boss wake 50 Cent, alisema hiyo ilikuwa ni beef ya muda mfupi, “ilidumu kwa muda wa mwaka mmoja au miwili hivi na ilinichukulia muda mwingi sana na ilinifrustrate mimi na watu wengi. Kwa hiyo nilipoanza kuandaa album ya tatu, ya pili na sasa nimeanza na hii ya nne nadhani busara kidogo ilitumika, na mimi natokea Los Angeles na sikujiingiza moja kwa moja katika huo mtego” alisema Game akimaanisha mtego wa hilo beef.
Akamaliza kusema anadhani hii inawahusisha zaidi fans wao na wakosoaji wao na kile kilichoko kati ya maadui wawili ambao walikuwa ni yeye na 50 Cent na kwamba sometimes asingeweza kucontrol hili.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates