Check Walter Chilambo alivyo chukua ml.50 BSS

Walter baada ya kukabidhiwa zawadi ya Milioni 50 alizojishindia
Usiku wa kuamkia leo Jumamosi Nov 10, 2012 ndio ilifanyika fainali ya shindano kubwa la kutafuta vipaji vya kuimba Tanzania Epic Bongo Star Search (EBSS), ambapo lilimuibua mshindi wa mwaka huu ambae ni Walter Chilambo kutoka Dar es salaam aliyejinyakulia zawadi ya shilingi Million 50 ya kitanzania iliyokuwa imeandaliwa kwa mshindi.



Shindano la mwaka huu lilionekana kuwa na ushindani mkubwa kutokana na uwezo mkubwa waliokuwa nao washiriki hasa waliofanikiwa kuingia hadi hatua ya 5 bora. 





Walter aliibuka mshindi baada ya kufanikiwa kuingia 2 bora na bibie Salma kutoka Zanzibar alietoa ushindani wa hali ya juu.


Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates