Noise Maker kwa DX ni kituo muhimu cha Roma akiwa Arusha, asema anapenda kufanya kazi na wasanii wa A.City.


Wengi waliousikia wimbo wa Roma wa 2030 walipata hisia kuwa kulikuwa na punch kwa A.City artists Over Tanga ambapo ndo sehemu anakotokea, ama waliposikia mistari kwenye mashairi ya wimbo wake mmoja akisema 'Hip Hop ina uwanja mpana usiseme tu iko R-Chuga'. Kama wewe ni mmoja wao utakuwa unakosea hivi na inabidi umsome tena Roma.
Kupitia ukurasa wake wa facebook ROMA ameonesha kuwa mara nyingi anapokuwa Arusha hupenda kupiga collabo na wasanii wa pande hizo, na kazi zote zinapikwa pale Noise Maker na producer DX, na moja kati ya ngoma zilizopikwa hapo inaitwa 'Ukweli' akiwa na Banx na Mo Plus.Kwa hali hiyo booth ya Noise Maker ni kituo muhimu sana kwa mshindi huyo wa tuzo ya mwana Hip Hop bora.
Hivi ndivyo alivyosema Roma kupitia ukurasa wake wa facebook na kuambatanisha na picha akiwa na Mo Plus na Banx Baba la Ukoo.
"KILA NIENDAPO ARUSHA (ARACHUGA)!!! HUPENDA KUFANYA NGOMA NA MANINJA WA KULE!! DX HUSIMAMIA MIZIGO YOTE HII
with ma ninja BAAAANXXXX na MO PLUS BABA LA UKOO
NGOMA INAITWA "UKWELI"
A.city "

R.O.M.A (Rhymes Of Magic Atraction) ndivyo anavyojiita na kulitafsiri jina lake, kila akitoa wimbo mashairi yake huwa na nguvu ya ajabu kuvuta attention ya wasikilizaji wake kitu ambacho kimesababisha watu wengi kuvutika na kununua wimbo wake 2030 kwa shillingi 3000 kwa njia ya email, lakini pia baada ya kuuachia tu uliongoza kwa kupakuliwa kwenye mtandao kwa hapa Tanzania.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates