TAHADHARI : USIKUBALI KUTAPELIWA :


Inazidi kudhihirika kuwa ANTHONY SHILLIYE LUCAS ambaye anadai kuwa ni Mhasibu wa kampuni inayoitwa SOCIAL CREDIT COMPANY ni TAPELI na MWIZI WA MTANDAO.

Hadi sasa amewatapeli watu wengi kwa kuwataka wamtumia fedha kiasi cha shs. 45,000/- kupitia namba ya MPESA 0756 310 988 (ANTHONY SHILLIYE) na TIGOPESA 0714 254 735 (ANTHONY LUCAS).

Mchezo anaofanya kusambaza habari zake za utapeli ni kupitia “INTERNET PHISING” ambapo anaiba user name na password za akaunti za facebook za watu mbalimbali na wakati mwingine kutengeneza akaunti feki ambazo huzitumia kuwashawishi watu kuhusu kuwepo kwa mikopo na kampuni hiyo.

Hadi sasa ameweza kuhaki iliyokuwa akaunti ya dar24 ambayo ilikuwa inaitwa DAR24.COM na pia ametengeneza akaunti feki ya Wema Sepetu: https://www.facebook.com/wema.sepetu.946?fref=ts na AirTel Tanzania https://www.facebook.com/pages/Airtel-Tanzania/438820529559726; ambazo amekuwa anazitumia kuwatapeli watu.


Kwahivi sasa Dar24 hatutoi mikopo na wala hatuijui hiyo kampuni. HIVYO MNATAHADHARISHWA KUTOKUAMINI UJUMBE WOWOTE WA MIKOPO KWENYE FACEBOOK ACCOUNT HIZO. Taarifa hizi pia ziko POLISI, TCRA na kwenye Kampuni za Simu.

Tushirikiane kwa kuwatahadharisha watu zaidi kukwepa mtego huu. Pia usifungue akaunti hii : http://www.socialcompany.wapka.mobi/index.html.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates