NEWS - Serikali yasisitiza dhamira yake kuhusu ndoa za utotoni

August 19 2016 Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto amefanya uzinduzi wa mradi wa kukusanya nguvu za pamoja kulinda haki za wasichana nchini Tanzania awamu ya II jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo Waziri Mwalimu amesisitiza dhamira ya Serikali ni kuendeleza jitihada za kufanya marekebisho ya sheria ya ndoa ya mwaka 1997, hususan katika kifungu 13 (1) cha sheria ya ndoa kinachoeleza kuwa umri wa mtoto wa kike kuolewa ni kuanzia miaka 15.

Aidha Waziri Mwalimu ametoa ufafanuzi zaidi kuhusu Serikali kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama kuu kuhusu sheria hiyo kuwa ni ili kupata maamuzi ya juu zaidi ambayo hayataweza kupingwa na mahakama nyingine ya chini.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates