Godzilla auponda mfumo wa elimu Tanzania




Rapper mwenye swagga za 50 Cent, Godzilla ameukosoa mfumo wa elimu uliopo nchini ambao anadai hautengenezi wataalam. Kupitia mtandao wa Facebook, Godzilla ameandika:

Mfumo wa Elimu Tanzania inabidi ubadilishwe. Elimu ndefu sana na haiko katika kutengeneza wataalam(Experts).

Mfano mtu kasoma hadi darasa la 7 akafeli na mtu aliyesoma hadi Form6 akafeli wote wanakuwa sawa coz hawaajiliwi #so miaka yote imepotea bure.

Zamani kulikuwa hadi na la 4 la mkoloni wazee wakifika la 4 wanamaliza sa hivi aje wazee?!

Fanyeni mfumo mzuri wa Elimu ili tuwe na wasomi wengi.

Mawazo mazuri Godzilla.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates