Iddi Azan: Bodi ya filamu imelala usingizi




Mbunge wa Kinondoni Iddi Azan ameiponda bodi ya filamu nchini kuwa imelala na hivyo kushindwa kufanya kazi yake.

Akichangia hoja bungeni kwenye mjadala wa  Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, amesema zipo filamu nyingi zinazoingia nchini zenye mambo machafu lakini hazichukuliwi hatua yoyote.

Amesema kuna mtindo umekuwa maarufu sana nchini wa kuingizwa kwa filamu za ngono zilizotengenezwa nje lakini makava yake yakiwa na picha za wasanii wa Tanzania.

Mbunge huyo ametaka apewe maelezo ya kutosha kutoka kwa wizara hiyo kama wasanii wa Tanzania wanaoonekana kwenye makava hiyo ndio waliocheza movie hizo.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates