Britney Spears, Taylor swift wamsogelea Oprah katika list ya wanawake wanaolipwa zaidi, Rihanna nafasi ya nne, Beyonce afichwa.

Oprah Winfrey

List ya wanawake wanaojihusisha na entertainment wanaolipwa mpunga mrefu zaidi duniani kwa ajili ya kazi zao kwa mwaka iliyotolewa na Forbes inaonesha kuwa Oprah Winfrey anayeendesha talk show anashikilia nafasi ya kwanza, ambapo kati ya may 2011 na may 2012 amepokea $ 165 million. Na imegundulika kuwa bado kuna mshahara mwingine hajapata, kwa hiyo hautajumuishwa kwenye pato la mwaka ujao, 2013 ili isiwe nafasi ya kumuongezea ushindi tena mwaka ujao kumbe kuna pato la mwaka huu bado analisubiria.

Britney Spears
Katika list hiyo nafasi ya pili imekamatwa na judge wa X Factor mwanadada Britney Spears, ambae yeye ameingiza mpunga wa ukweli kiasi cha $58 million ndani ya mwaka mmoja. Kwa mujibu wa Forbes Spears alimake mkwanja mrefu sana kupitia album yake na hasa kupitia tour ya album hiyo aliyoibatiza “Femme Fatale tour”, na  alijazilishia kwa mkataba mnono wa kuendesha X Factor ambao ni $15 alizozisign.
Taylor Swift
Nafasi ya tatu imekamatwa na mwanadada Taylor Swift ambae ana historia ya aina yake na MTV VMAs, alipovamiwa jukwaani na Kanye West, na hili tukio liliwafanya watu wengi zaidi kutega masikio kwa huyu mwanadada mwenye umri wa miaka 22 hivi. Yeye amemfata kwa karibu sana Briteney Spears kwa kuingiza $57 millioni kwa mwaka kama pato halisi. Huyu ni mwanadada mwenye umri mdogo zaidi kwenye hii list na tour yake ya Speak Now ilichangia kwa kiasi kikubwa sana pato lake lakini pia ngoma kibao kali alizoachia ikiwemo ile safe &sound. Na mwezi huu anatarajia kuachia album yake inayoitwa Red. Kumbuka wimbo wake wa kwanza ulikaa kwenye nafasi za juu sana za Billboard’s Hot 100 chart kwa muda wa wiki tatu.

Rihanna
Nafasi ya nne imekamatwa na the R&B Queen Rihanna, lakini hapa amefungana na mwanadada Ellen DeGeneres wote wakiwa wameingiza kiasi cha $53 million.

Nafasi ya tano imekatwa na Lady Gaga na  jaji wa zamani wa American pop Idol Jeniffer Lopez, wakali hawa wamefungana pia na wameingiza mpunga kiasi cha $52 million kwa kipindi cha mwaka mmoja. Gaga album yake iliyoambatana na tour ya Born This Way imemsaidia kufika hapo.
Wakati majina yanaendelea kushuka, list ilifungwa na supper modal Gisele Bundchen ($45 million) Katy Perry ($45 million) na Judge Judy wa TV show ($45 million).

Hadi list inafungwa hakuna jina la mama Blue Ivy, mwimbaji  Beyonce Knowles Carter hata kwenye top five japo wengi walimtegemea hata katika top three. Kibongobongo tungesema hapa wanawake wenzake waburudishaji wamemficha.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates