Nick Minaj ambwatukia Mariah Carey, amtishia “I’m gonna knock you out”

Nick Minaj

Wiki chache baada ya Mariah Carey kukanusha tetesi kuwa alikuwa na beef na Young Money Queen Nick Minaj ambae ni jaji mwenzake kwenye American Idol sasa mambo yamekuwa tofauti baada ya video yenye picha tofauti kabisa na kile kilichoelezwa na Carey kusambaa kwenye mitandao.
Video hiyo inaonesha Nick Minaj akiwa kakasirika na anampa makavu live Mariah Carey, tukio hili limetokea wakati wanaendelea na kazi yao ya kujaji washiriki mbalimbali na safari hii walikuwa Charlotte, North Carolina.
Mtu mmoja ambae alishuhudia live tukio hilo amesema kuwa Nick Minaj alionekana kupandisha mzuka na kufikia hatua ya kumtishia the R&B diva Mariah Carey na kusema “I’m gonna knock you out”.
Chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa Nick Minaj aliongea kwa sauti ya juu sana na kumtolea matusi makali Mariah Carey akisema “I told them, I’m not f***kin’ putting her f**kin’ highness there.”  Lakini hii sehemu haikushikwa na lensi ya camera hiyo iliyokuwa inachukua matukio ya American Idol.
Inasemekana kuwa hii varangati ilitokea baada ya kutofoutiana sana katika maamuzi kwa washiriki walio-perform siku hiyo. Wakati hayo yanatokea, Nick Minaj na Mariah Carey walikuwa wamekaa kwenye meza ya majaji, na jaji mwenzao Keith akiwa amekaa katikati yao na Randy Jackson akiwa amekaa mwishoni upande wa Mariah Carey.
Kutokana na hali hiyo watayarishaji wa American Idol iliwalazimu kusimamisha performance ya siku hiyo ili majaji hawa wacool down kwanza. Hali hii inaonekana kuwatishia waandaji wa American Idol na wana wasiwasi kama Nick Minaj na Mariah Carey watadumu kwa muda mrefu wakiwa wanafanya kazi yao pamoja kama majaji wa American Idol.

Mariah Carey
Katikati ya mwezi September iliripotiwa kuwa Nick Minaj na Mariah Carey hawana maelewano mazuri, na mtu mmoja ambae ni mfatiliaji wa mambo ya muziki Marekani alisema hata Mariah Carey alipopigiwa simu kuambiwa kuwa Nick Minaj ndo atakuwa jaji mwenzake kati ya wale wanne alikata simu.
Lakini September 17 ambapo MTV ilienda New York pale ambapo American Idol ilikuwa imeanza na ikafanyika kwa siku mbili, ili kujionea nini kilikuwa kinaendelea kati ya Mariah Carey na Nick Minaj, na walipouliza kuhusu kutoelewana, wote walikuwa wanatabasamu kama vile walisikia utani hivi, na Mariah Carey akaonesha kushangazwa na taarifa hizi jinsi zilivyosambaa kwa haraka ndani ya muda mfupi sana, na akamaliza kwa kusema "It's fun, it's music, it's singing, it's laughter," na Nick Minaj akawa anatikisa kichwa kuonesha anasapoti alichokuwa anasema Mariah Carey.

Wajuzi wa mambo walisema time will tell sasa kila kitu kinaanza kuonekana hadharani, chanzo kabisa cha kutoelewana kwa wawili hawa bado hakijajulikana kwa sababu kama Mariah Carey alikata simu pale tu aliposikia jaji mwenzake atakuwa Nick Minaj, basi chanzo sio kutoelewana katika maamuzi ya ujaji wao, there must be a long term factor.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates