Katika kile
kinachoonekana kuwa Lady Jaydee ameanza kuogopa moto wa bendi mpya ya SkyLight
inayoongozwa na Aneth Kushaba, kiongozi huyo wa bendi ya Machozi ameitupia madongo
bendi hiyo.
“Its not
about making noise na mabango. Debe likiwa tupu ni tupu tu. Its all about what
u can do,” ametweet Jaydee mchana wa Jumamosi.
Tweet hiyo
iko wazi kwakuwa anazungumzia mabango yanayoonekana kwenye mitaa mbalimbali ya
jiji la Dar es Salaam yakiwa yamebebwa na akinadada waliolipwa kufanya kazi
hiyo.
Hivi karibuni
aliyekuwa muimbaji wa bendi ya Machozi, Sam Machozi alihamia kwenye bendi hiyo inayokuja
juu nchini ambayo Eid mosi na Pili itapiga show Girrafe Ocean View Hotel.
Post a Comment