HIVI NDIVYO JUX ALIVYOMLIPA DIAMOND KWA KUONESHA JEURI YA PESA

Muimbaji wa Uzuri Wako, Jux anafahamika kwa kuishi maisha ya kifahari kama vile kuvaa cheni za dhahabu, nguo na viatu vya bei ghali na vitu vingine, hali ambayo imekuwa ikimfanya aonekane kutofanya muziki kwa njaa bali kama hobby tu. Wale wanaomfuata Instagram, watakuwa wanajua namna anavyopenda ‘kubrag’ kwa kuweka picha zinazoishia kuwaumiza roho wengi.
Msanii huyo wa RnB wa kundi la Wakacha, ameenda mbali zaidi leo kwa kupost picha ya vitita vinne vikubwa vya noti za dola 100 za Kimarekani zikiwa zimewekwa kwenye mapaja yake pamoja na simu ya iPhone inayoonekana kuwa ya dhahabu aka ‘gold plated iPhone’.
“Money brings happiness power respect problems enemies and alot of fakefriends but its good to have it morng instagram,” ameandika mkali huyo.
“Uuwiiii jamani jux mbona unatutempt aseeeh,” ameandika mmoja wa followers wake.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates