PICHA - ASHLEY COLE ASAINI ROMA

Beki wa zamani wa Chelsea Ashley Cole amejiunga na klabu ya Roma ya Italia kwa mkataba ya miaka miwili.

Roma ime 'tweet' picha ya Cole na kuthibitisha kupitia tovuti yao kuwa mchezaji huyo amesaini mkataba hadi mwaka 2016.
Ashley Cole ameichezea Chelsea kwa miaka minane, akishinda ligi kuu mwaka 2010 na Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2012.
Pia alishinda vikombe vinne vya FA na Chelsea, kuongeza vitatu alivyoshinda akiwa na Arsenal ambayo alishinda nayo makombe mawili ya ligi pia.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates