Latest Updates

Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

NEWS- WATANZANIA WANAOISHI NCHINI UK WAMEFANYA HIKI ILI KUSAIDIA WATU WENYE UALBINO

7:18 PM
 Jumamosi ya tarehe 15/10 Watanzania wanaoishi Uingereza walifanya hafla  kuchangisha fedha kwa wajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino,
hafla hiyo iliyofanyika  Stratford City hall, jijini London
 ilihudhuriwa na bwana Josephat Toner kutokea chama cha albino Tanzania,

PICHA - WANAUME WA JAPANI WAMESOMA KOZI HII ILI KUVUTIA WANAWAKE

10:29 PM

Najua kuna watu wangu ambao sasa wapo kwenye mchakato wa kuoa au ndio wanatafuta mtu ambaye wataishi nao, lakini inawezekana kumekuwa na changamoto, Sasa leo September 20 2016 nakusogezea hii inayotokea nchini Japan ambapo wanaume ambao bado hawajaoa wanahudhuria kozi ya kulea watoto ili kumvutia mwanamke zaidi.

Bachelor hao wa kijapan wamehudhuria kozi ya kulea watoto ili kuongeza nafasi ya wao kupata wapenzi, Mwalimu wa kozi hiyo Takeshi Akiyama amesema lengo la kozi hiyo ambayo imeandaliwa na Ikumen University ni ili kusaidia mtu ambaye hajaoa kupata mke.

Masaya Kurita (31) bachelor anayeishi Tokyo Japan ameanza kozi baada ya kutafuta mke kwa miezi sita iliyopita, Aidha anaamini kuwa kufanya mazoezi ya kulea mtoto kwa kutumia plastiki kunaboresha nafasi yake ya  yeye kukukbalika kwa mpenzi .

NEWS - MTEMVU ASHINDWA KESI YA UBUNGE TEMEKE

10:26 PM

Aliyekuwa Mbunge wa Temeke (CCM) Abbas Mtemvu, ameshindwa kesi ya uchaguzi dhidi ya Abdallah Mtolea(CUF) aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi wa Oktoba mwaka jana.

Mtemvu aliyekuwa akitetea kiti hicho katika uchaguzi Mkuu wa mwaka jana alifungua kesi  katika  Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akipinga matokeo yaliyompa ushindi  Mtolea.
Pamoja na mambo mengine akidai kuwa kura  za baadhi ya vituo vya kupigia kura hazikujumlishwa katika matokeo ya jumla.

Hata hivyo Mahakama Kuu katika hukumu yake iliyotolewa   na Jaji Issa Maige aliyekuwa akisiliza kesi hiyo imetupilia mbali madai ya Mtemvu na badala yake imemthibitisha Mtolea kuwa mbunge halali wa jimbo hilo.

Katika hukumu hiyo Jaji Maige amesema kuwa Mtemvu ameshindwa kuthibitisha madai yake jinsi yalivyoathiri ushindi wa mbunge huyo, huku akisema kwamba kasoro alizokuwa akizilalamikia Mtemvu hakuathiri ushindi wa mbunge huyo.

News wasiokua na uraia wajadiliwe

10:23 PM


Tanzania  imeitaka jumuiya ya  kimataifa   kujadili  tatizo  la  uwepo wa watu  ambao si raia wa nchi  yoyote ile.

Pendekezo hilo limetolewa siku ya  Jumanne na Waziri wa Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Dkt. Augustine Mahiga ( Mb)    katika  mkutano     wa  Kilele wa  viongozi  kuhusu wakimbizi.

Mkutano huo  uliandaliwa na  Rais wa Marekani Barack Obama  kwa  ubia na nchi za  Ethiopia, Jordan, Mexico, Sweden, Canada  na Ujerumani  ambapo nchi  60  zilialikwa,45 kati ya zilizoalikwa ikiwamo   Tanzania    zilitoa ahadi ya  namna moja ama  nyingine. 

Nchi  hizo ni zile ambazo kwa namna moja ama nyingine   zimekuwa zikiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi,  zimekuwa nchi za mpito kwa wakimbizi, au zimekuwa  zikitoa misaada   ikiwamo ya  hali na mali pamoja na kuwapatia uraia, ajira na  misaada ya kibinadamu.

Lengo kuu la mkutano  huo wa  viongozi kuhusu wakimbizi lilikuwa ni kwa nchi kutoa ahadi mpya ambazo  kwayo  zitasaidia katika  kuwapatia fursa za ziada  wakimbizi ili  pamoja na mambo mengine kuwapunguzia changamoto zinazowakabili na kuwafanya wajisikie na kujiona  kuwa  nao ni  binadamua kama  binadamu  wengine.

Akizungumza kwa  niaba ya Serikali,   Waziri Mahiga, amesema, Tanzania  kutokana na jiografia ya nchi hiyo  ilivyo imejikuta  mara kwa mara ikiwa ni kimbilio  la wakimbizi kutoka  nchi jirani.

Akawaeleza  washiriki wa mkutano huo, kwamba, suala la  Tanzania  kuwahifadhi  wakimbizi ni la kihistoria na  halikuanza  jana au juzi.

“ Tanzania kutokana na jiografia yake imejikuta  ikiwa ni kimbilio wa watu wanaotafuta salama ya maisha yao. Tumekuwa  tukiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi  tangu miaka  ya 60.  Na  tunatekeleza   jukumu hilo kwa kuzingatia sheria  za kimataifa na mikataba ya kimataifa, na sheria zetu za ndani” akasema Mahiga.

 Na kuongeza kwamba, Tanzania itaendelea na jukumu hilo pale itakapopashwa  kufanya   hivyo kwa  kufuata na kuzingatia sheria  za nchi na  sheria za kimataifa.

CHIWILE INC IS BACK

7:42 AM

Chiwileinc is Back! Kaa tayari

NEWS - VIPENGELE TUNZO ZA EATV AWARDS VIKO HAPA

11:45 AM

Vipengele vya tuzo mpya zilizoanzishwa na kituo cha runinga cha East Africa Televisheni, EATV Awards, vimetangazwa Ijumaa hii.

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Mkuu wa masoko wa kituo EATV,Roy Mbowe alisema tuzo hizo zitakuwa na vipengele 10 zitakazohusisha muziki, filamu na tuzo moja ya heshima.
Vipengele hivyo ni:

1. Mwanamuziki bora wa kiume
2. Mwanamuziki bora wa kike
3. Mwanamuziki bora chipukizi
4. Kundi bora la muziki
5. Video bora ya muziki
6. Wimbo bora wa mwaka
7. Muigizaji bora wa kiume
8. Muigizaji bora wa kike
9. Filamu bora ya mwaka
10. Tuzo ya heshima itakayotolewa kwa mtu au kampuni iliyochangia kwa kiasi kikubwa katika kazi za muziki.

Mbowe amesema kazi za sanaa zitakazoruhusiwa kuingia kwenye vipengele ni zile zilizotoka kuanzia Julai 1 2015 – 30 Juni 2016. Tofauti na tuzo zingine, wasanii wanaotaka kushiriki watalazimika kujaza fomu za kutaka kutajwa kwenye tuzo na kuwasilisha kazi husika ambapo mchakato wa uchambuzi wa kazi hizo utachukua kipindi cha mwezi mmoja kabla ya majina yaliyoingia kwenye tuzo hizo kutajwa na kuanza kupigiwa kura.

Hata hivyo amedai kuwa pamoja na wananchi kupiga kura, kutakuwepo na jopo la majaji litakaloshiriki kupata washindi. Tuzo hizo zinazodhaminiwa na kampuni ya Vodacom, zitatolewa December 10 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

News- bila wivu hakuna mapenzi jux

10:26 AM

Msanii Jux ambaye sasa ni mpenzi wa Vanessa Mdee amefunguka na kusema kuwa wimbo wake mpya 'Wivu' ambao unafanya vizuri kwa sasa hajaimba kwa ajili ya mpenzi wake Vanessa Mdee.

bali ameimba wimbo huo kutokana na hisia kwani jambo hilo linawakuta wengi ambao wanapendana kweli katika mahusiano yao ya kila siku.

Jux akizungumza kwenye kipindi cha ENEWZ ya EATV alidai kwenye mapenzi kama hakuna wivu kati ya wawili wapendanao hapo kunakuwa hakuna mapenzi ya kweli kati yao kwani wivu ndiyo ishara ya upendo wa kweli.

"Wimbo wa Wivu ni matukio ya kimapenzi ambayo yanatokea kwa watu wengi ila siyo kama nimejiimbia mimi, unajua kabla sijarekodi wimbo ule tukiwa studio niliwauliza wakina Bob Manecky na wengine jamanii mnadhani 'idea' hii inaweza kuwa sawa ndipo hapo wakaniambia ni wazo zuri kwani kwenye mapenzi bila uwepo wa wivu kuna kuwa hakuna mapenzi ya kweli, ndiyo hapo nikajua kumbe suala hili linawagusa watu wengi" alisema Jux.

Mbali na hilo Jux amesema kuwa hivi sasa muzuki unakuwa kama haupo kutokana na ukweli kwamba watu wanatanguliza life style mbele kuliko hata kazi zao na ndiyo maana wasanii wengi wakitaka kutoa kazi zao wanafanya mambo mbalimbali kutafuta kiki ili waweze kutambulisha kazi zao hizo.

"Sipendi sana kuulizwa maswali juu ya Vanessa napenda niulizwe maswali juu ya kazi zangu mimi kama msanii, ili nitangaze kazi zangu mimi ndiyo maana kuna vitu saizi sisi tunavikwepa kwa makusudi, tunataka kurudisha muziki hivyo mambo ya kiki, life style tunataka yakae pembeni" alisema Jux

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates