MAALIM SEIF AMTEMBELEA BI KIDUDE


Bi Fatma bint Baraka maarufu Bi Kidude akisisitiza kwamba yeye ni mzima hasa kwa wale waliojaribu kumzushia kwamba amefariki ila miguu ndiyo inamsumbua kwa sasa. 


Makamu wea Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akiomba dua pamoja na msaniii mkongwe wa muziki wa Taarab nchini Bi Fatma bint Baraka alipomtembelea. 
 


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amefanya ziara ya kuwatembelea wagonjwa na wazee kwa ajili ya kuwapa pole na kuwafariji katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.
Miongoni mwa wagonjwa waliotembelea na Maalim Seif ni msanii maarufu hapa Zanzibar, Bi. Fatma binti Baraka maarufu Bi. Kidude ambaye anasumbuliwa na maradhi ya miguu kwa wiki kadhaa sasa.

Bi. Kidude akizungumza na Maalim Seif huko nyumbani kwa mwanawe Kihinani, Wilaya ya Magharibi Unguja, alimueleza kuwa anasumbuliwa na maradhi ya miguu, lakini amekuwa akifanya shughuli zake nyingi za kawaida.
Hata hivyo, Bi. Kidude alisema amesikitishwa sana na kitendo cha baadhi ya watu kueneza uvumi kwamba amefariki wakati bado ni mzima na anafanya shughuli zake kama kawaida.
Alimueleza Maalim Seif kuwa kitendo cha watu hao licha ya kumsikitisha yeye binafsi, pia kimesababisha usumbufu na hofu kubwa miongoni mwa jamii na baadhi ya watu ambao walilazimika kufunga safari kuja Zanzibar kutoka nchi mbali mbali. “Kuna watu wameeneza taarifa za uongo kwamba nimekufa, wapo watu waliofunga safari kutoka nchi tafauti kuja Zanzibar, lakini walipofika walishangaa kuniona nipo hai”, alisema Msanii huyo maarufu wa muziki wa taarab hapa Zanzibar na Afrika Mashariki.

Share this:

Post a Comment

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates