Latest Updates

Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

NEWS- WATANZANIA WANAOISHI NCHINI UK WAMEFANYA HIKI ILI KUSAIDIA WATU WENYE UALBINO

7:18 PM
 Jumamosi ya tarehe 15/10 Watanzania wanaoishi Uingereza walifanya hafla  kuchangisha fedha kwa wajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi albino,
hafla hiyo iliyofanyika  Stratford City hall, jijini London
 ilihudhuriwa na bwana Josephat Toner kutokea chama cha albino Tanzania,

PICHA - WANAUME WA JAPANI WAMESOMA KOZI HII ILI KUVUTIA WANAWAKE

10:29 PM

Najua kuna watu wangu ambao sasa wapo kwenye mchakato wa kuoa au ndio wanatafuta mtu ambaye wataishi nao, lakini inawezekana kumekuwa na changamoto, Sasa leo September 20 2016 nakusogezea hii inayotokea nchini Japan ambapo wanaume ambao bado hawajaoa wanahudhuria kozi ya kulea watoto ili kumvutia mwanamke zaidi.

Bachelor hao wa kijapan wamehudhuria kozi ya kulea watoto ili kuongeza nafasi ya wao kupata wapenzi, Mwalimu wa kozi hiyo Takeshi Akiyama amesema lengo la kozi hiyo ambayo imeandaliwa na Ikumen University ni ili kusaidia mtu ambaye hajaoa kupata mke.

Masaya Kurita (31) bachelor anayeishi Tokyo Japan ameanza kozi baada ya kutafuta mke kwa miezi sita iliyopita, Aidha anaamini kuwa kufanya mazoezi ya kulea mtoto kwa kutumia plastiki kunaboresha nafasi yake ya  yeye kukukbalika kwa mpenzi .

NEWS - MTEMVU ASHINDWA KESI YA UBUNGE TEMEKE

10:26 PM

Aliyekuwa Mbunge wa Temeke (CCM) Abbas Mtemvu, ameshindwa kesi ya uchaguzi dhidi ya Abdallah Mtolea(CUF) aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi wa Oktoba mwaka jana.

Mtemvu aliyekuwa akitetea kiti hicho katika uchaguzi Mkuu wa mwaka jana alifungua kesi  katika  Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akipinga matokeo yaliyompa ushindi  Mtolea.
Pamoja na mambo mengine akidai kuwa kura  za baadhi ya vituo vya kupigia kura hazikujumlishwa katika matokeo ya jumla.

Hata hivyo Mahakama Kuu katika hukumu yake iliyotolewa   na Jaji Issa Maige aliyekuwa akisiliza kesi hiyo imetupilia mbali madai ya Mtemvu na badala yake imemthibitisha Mtolea kuwa mbunge halali wa jimbo hilo.

Katika hukumu hiyo Jaji Maige amesema kuwa Mtemvu ameshindwa kuthibitisha madai yake jinsi yalivyoathiri ushindi wa mbunge huyo, huku akisema kwamba kasoro alizokuwa akizilalamikia Mtemvu hakuathiri ushindi wa mbunge huyo.

News wasiokua na uraia wajadiliwe

10:23 PM


Tanzania  imeitaka jumuiya ya  kimataifa   kujadili  tatizo  la  uwepo wa watu  ambao si raia wa nchi  yoyote ile.

Pendekezo hilo limetolewa siku ya  Jumanne na Waziri wa Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Dkt. Augustine Mahiga ( Mb)    katika  mkutano     wa  Kilele wa  viongozi  kuhusu wakimbizi.

Mkutano huo  uliandaliwa na  Rais wa Marekani Barack Obama  kwa  ubia na nchi za  Ethiopia, Jordan, Mexico, Sweden, Canada  na Ujerumani  ambapo nchi  60  zilialikwa,45 kati ya zilizoalikwa ikiwamo   Tanzania    zilitoa ahadi ya  namna moja ama  nyingine. 

Nchi  hizo ni zile ambazo kwa namna moja ama nyingine   zimekuwa zikiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi,  zimekuwa nchi za mpito kwa wakimbizi, au zimekuwa  zikitoa misaada   ikiwamo ya  hali na mali pamoja na kuwapatia uraia, ajira na  misaada ya kibinadamu.

Lengo kuu la mkutano  huo wa  viongozi kuhusu wakimbizi lilikuwa ni kwa nchi kutoa ahadi mpya ambazo  kwayo  zitasaidia katika  kuwapatia fursa za ziada  wakimbizi ili  pamoja na mambo mengine kuwapunguzia changamoto zinazowakabili na kuwafanya wajisikie na kujiona  kuwa  nao ni  binadamua kama  binadamu  wengine.

Akizungumza kwa  niaba ya Serikali,   Waziri Mahiga, amesema, Tanzania  kutokana na jiografia ya nchi hiyo  ilivyo imejikuta  mara kwa mara ikiwa ni kimbilio  la wakimbizi kutoka  nchi jirani.

Akawaeleza  washiriki wa mkutano huo, kwamba, suala la  Tanzania  kuwahifadhi  wakimbizi ni la kihistoria na  halikuanza  jana au juzi.

“ Tanzania kutokana na jiografia yake imejikuta  ikiwa ni kimbilio wa watu wanaotafuta salama ya maisha yao. Tumekuwa  tukiwapokea na kuwahifadhi wakimbizi  tangu miaka  ya 60.  Na  tunatekeleza   jukumu hilo kwa kuzingatia sheria  za kimataifa na mikataba ya kimataifa, na sheria zetu za ndani” akasema Mahiga.

 Na kuongeza kwamba, Tanzania itaendelea na jukumu hilo pale itakapopashwa  kufanya   hivyo kwa  kufuata na kuzingatia sheria  za nchi na  sheria za kimataifa.

CHIWILE INC IS BACK

7:42 AM

Chiwileinc is Back! Kaa tayari

NEWS - VIPENGELE TUNZO ZA EATV AWARDS VIKO HAPA

11:45 AM

Vipengele vya tuzo mpya zilizoanzishwa na kituo cha runinga cha East Africa Televisheni, EATV Awards, vimetangazwa Ijumaa hii.

Akizungumza kwenye kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Mkuu wa masoko wa kituo EATV,Roy Mbowe alisema tuzo hizo zitakuwa na vipengele 10 zitakazohusisha muziki, filamu na tuzo moja ya heshima.
Vipengele hivyo ni:

1. Mwanamuziki bora wa kiume
2. Mwanamuziki bora wa kike
3. Mwanamuziki bora chipukizi
4. Kundi bora la muziki
5. Video bora ya muziki
6. Wimbo bora wa mwaka
7. Muigizaji bora wa kiume
8. Muigizaji bora wa kike
9. Filamu bora ya mwaka
10. Tuzo ya heshima itakayotolewa kwa mtu au kampuni iliyochangia kwa kiasi kikubwa katika kazi za muziki.

Mbowe amesema kazi za sanaa zitakazoruhusiwa kuingia kwenye vipengele ni zile zilizotoka kuanzia Julai 1 2015 – 30 Juni 2016. Tofauti na tuzo zingine, wasanii wanaotaka kushiriki watalazimika kujaza fomu za kutaka kutajwa kwenye tuzo na kuwasilisha kazi husika ambapo mchakato wa uchambuzi wa kazi hizo utachukua kipindi cha mwezi mmoja kabla ya majina yaliyoingia kwenye tuzo hizo kutajwa na kuanza kupigiwa kura.

Hata hivyo amedai kuwa pamoja na wananchi kupiga kura, kutakuwepo na jopo la majaji litakaloshiriki kupata washindi. Tuzo hizo zinazodhaminiwa na kampuni ya Vodacom, zitatolewa December 10 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

News- bila wivu hakuna mapenzi jux

10:26 AM

Msanii Jux ambaye sasa ni mpenzi wa Vanessa Mdee amefunguka na kusema kuwa wimbo wake mpya 'Wivu' ambao unafanya vizuri kwa sasa hajaimba kwa ajili ya mpenzi wake Vanessa Mdee.

bali ameimba wimbo huo kutokana na hisia kwani jambo hilo linawakuta wengi ambao wanapendana kweli katika mahusiano yao ya kila siku.

Jux akizungumza kwenye kipindi cha ENEWZ ya EATV alidai kwenye mapenzi kama hakuna wivu kati ya wawili wapendanao hapo kunakuwa hakuna mapenzi ya kweli kati yao kwani wivu ndiyo ishara ya upendo wa kweli.

"Wimbo wa Wivu ni matukio ya kimapenzi ambayo yanatokea kwa watu wengi ila siyo kama nimejiimbia mimi, unajua kabla sijarekodi wimbo ule tukiwa studio niliwauliza wakina Bob Manecky na wengine jamanii mnadhani 'idea' hii inaweza kuwa sawa ndipo hapo wakaniambia ni wazo zuri kwani kwenye mapenzi bila uwepo wa wivu kuna kuwa hakuna mapenzi ya kweli, ndiyo hapo nikajua kumbe suala hili linawagusa watu wengi" alisema Jux.

Mbali na hilo Jux amesema kuwa hivi sasa muzuki unakuwa kama haupo kutokana na ukweli kwamba watu wanatanguliza life style mbele kuliko hata kazi zao na ndiyo maana wasanii wengi wakitaka kutoa kazi zao wanafanya mambo mbalimbali kutafuta kiki ili waweze kutambulisha kazi zao hizo.

"Sipendi sana kuulizwa maswali juu ya Vanessa napenda niulizwe maswali juu ya kazi zangu mimi kama msanii, ili nitangaze kazi zangu mimi ndiyo maana kuna vitu saizi sisi tunavikwepa kwa makusudi, tunataka kurudisha muziki hivyo mambo ya kiki, life style tunataka yakae pembeni" alisema Jux

NEWS- watakao sambaza Ky kukiona

4:17 AM

MASHIRIKA yasiyo ya kiserikali (NGOs) ambayo yatabainika  yanaendelea   kusambaza vilainishi kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, yatafutiwa usajili.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu aliyaandika hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa ‘facebook’.

Alisisitiza kuwa serikali italisimamia suala hilo kwa ukamilifu.

“Sijapiga marufuku matumizi ya vilainishi, ukweli nimepiga marufuku mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) kununua na kusambaza vilainishi kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi na wanaume wenzao na sababu nimeshazieleza,” aliandika na kuongeza:

“Na nafurahi kuwajulisha kuwa tayari baadhi ya mashirika hayo yameanza kutekeleza agizo hili kwa   kuondoa vilainishi kwenye miradi yao. Nayapongeza sana. Niendelee kuyataka mashirika mengine kutii agizo hili ambalo tutalisimamia kwa ukamilifu.

“Serikali haitasita kuchukua hatua ikiwamo kuyafutia usajili mashirika yanayoendelea na miradi ya kusambaza vilainishi kwa wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja”.

Aliyataka mashirika hayo kushirikiana na serikali kupambana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kujikita kwenye afya nyingine  inayozingatia sheria za nchi  na mila na desturi za Watanzania.

Akizungumza Dar es Salaam hivi karibuni, Waziri Ummy alisema uamuzi huo umechukuliwa baada ya kubaini matumizi ya vilainishi hivyo yanachochea kuongezeka  vitendo vya ushoga ambavyo ni kinyume na sheria za nchi.

“Lengo pia ni kudhibiti maambukizi ya VVU kwa sababu katika   wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, asilimia 23 tayari wana maambukizi hayo.

“Tumebaini baadhi ya wadau wanaotekelezeka shughuli za makundi maalum wamekuwa wakikiuka taratibu za  utendaji na kusambaza vilainishi hivyo.

Awali agizo hilo lilizua mjadala mkubwa katika mitandao ya  jamii, wengi wakikosoa uamuzi huo wa Serikali kupiga marufuku vilainishi hivyo.

Walisema  kwamba vinatumika katika mambo mengine mtambuka hususan hospitalini huku wengine wakisema viendo vya ushoga havichangiwi na kuwapo   vilanishi bali ni mmomonyoko wa maadili uliotamalaki nchini

News- ngumbe & Salu T kuja na ngoma ya pamoja

2:26 PM

Baada ya kila mmoja kufanya poa kwenye ngoma zake artist toka lebo ya mandev records  wameamua kuja na muunganiko usio rasmin baada ya kuamua kufanya ngoma ya pamoja.
Wakiongea na chiwileinc Ngumbe amesema lengo ni kuchanganya mziki wa hip hop wenye ladha tofauti

"Unajua Salu t anafanya hardcore Mimi nafanya comecial  tumeona iv vitu tukiviweka pamoja vitaleta kitu tufauti kwa mashabiki wetu"

NEWS - Sirudi tena nyuma: Nuhu Mziwanda

7:53 PM
Licha ya maneno hayo kutoka kwa msanii huyo lakini baada ya kuachana na Shilole amekuwa akimshutumu mara kadhaa ikiwemo kutokuwa mwaminifu katika uhusiano wao na juzi kati alifunguka kuhusu kumfumania na Madee, madaia ambayo Madee aliyakanusha.

NEWS - Mesen Selecta asakwa na Polisi

7:48 PM
Akizungumza na eNewz Masopu sopu alisema kuwa alifanya ngoma na Mesen lakini mwisho wa siku Mtayarishaji huyo alikuwa kama anataka kumuingiza mjini baada ya kumuomba pesa kwa mara ya pili.

Panya anayegundua mabomu

1:06 AM

Panya anayegundua mabomu Afrika
'Panya mwokozi wa maisha'
Shirika moja lisilo la kiserikali la Ubelgiji APOPO limeanza kuwafundisha panya namna ya kutambua mabomu yaliyofukiwa ardhini. Panya hao ambao ni wakubwa kuliko panya wa kawaida wanafanyiwa majaribio Morogoro Tanzania .Inaaminika wanauwezo mkubwa wa kunusa kuliko mbwa. Hii inatokana na kuwa pua zao zipo karibu na ardhi,hali ambayo inawasaidia katika kazi yao ya utambuzi wa mabomu

Grandpa yamnasa Kenrazy

10:27 AM
Lebo ya muziki inayokuwa kwa kasi sana Afrika Mashariki, Grandpa kutoka Kenya, imefanya hatua nyingine ya nguvu kwa kumsaini nyota mwingine mkali wa muziki wa nchi hiyo, Kenrazy ambaye sasa anaungana na timu hiyo ambayo siku hadi siku inajizolea heshima kwa kazi nzuri inazofanya.

BAADA YA JOBFIRE KURUDI KWAO MOSHI NA KUSEMA MZIKI MGUMU TOWN SOMA ALICHO AMBIWA NA HAMMER Q

11:59 AM
hammerq  Fire ?? Katika maisha hakuna kitu kibaya km kukata tamaa, na ukumbuka xana maneno yangu kwamba Askari hatakiwi kurudi nyuma wakati wa vita anatakiwa asonge mbele kupambana na maadui sababu bila ya kupambana hawezi patikana mtu anaeitwa SHUJAA huwezi itwa shujaa kama hujapambana ,FIRE unatakiwa kurudi twn kuja kukamilisha melengo yako, mziki sio lelemama mwanangu unahitajika ukaze roho na misuli yote mwilini tuliza akili yako fire mziki unaujuwa na unauweza ila jifunze xana kupigana na moyo wakukata tamaa kumbuka mafanikio hayaji kwa siku moja

Jobfire Mkali nimekuelewa baba yangu ila usijali kuna mazingira nayatengeneza ili nipate kujiweka ktk nafasi fulan baba yangu najua unataman sana kuona mwanao nikifika mbali kimuziki ila ucjal baba yangu

Keko amzingua Linex?

9:43 AM
Kufuatia maswali mengi ya mashabiki wa muziki kuhusiana na kinachoendelea baada ya Msanii Linex hapo awali kutangaza kufanya kolabo na msanii mkubwa wa Uganda Keko, jambo ambalo halijafanyika, Linex ameongea na eNewz kufafanua juu ya mchongo huu.
 
Linex ameweka wazi kuwa, ratiba ya kwake pamoja na ya Keko ambazo zimekuwa na mambo mengi ndiyo kikwazo kikubwa ambacho kimefanya mchongo huu kuwa haujakamilika mpaka hivi sasa.
 
Msanii huyu ameeleza zaidi kuwa, Amekwishafanya jitihada za mara kwa mara kuwasiliana na Keko kumuuliza amefikia wapi na kukamilisha kipande chake kilichobakia ambapo kutokana na mambo mengi, Msanii huyu kutoka Uganda bado hajaweza kufanya kipande chake.
 
Linex amesema kuwa kwa sasa ameamua kutulia hadi msanii huyu wa Uganda atakapoamua kumalizia sehemu yake mwenyewe kwasababu kolabo hii inaumuhimu kwa pande zote mbili kwa kuwa yeye kama Linex ni msanii mkubwa hapa Tanzania, na Keko ni mkubwa kwa upande wa Uganda.

HATIMAYE MTANZANIA FEZA KESSY ATOLEWA KATIKA JUMBA LA BBA

11:55 AM

Mwasiti, Shetta watoa usia

11:27 AM
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanaofanya poa Hapa Tanzania, Mwasiti Almasi pamoja na Shetta ambaye kwa sasa yupo huko Kahama kwaajili kuwapa wananchi burudani ya Eid, Leo hii katika siku hii ya sikukuu ya Eid el Fitri kwa waislamu sehemu mbalimbali duniani, wamekuwa na ujumbe na wosia mzito kwa waamini wa dini hii ambao pia ni wapenzi wa burudani.

Mansu Li kutambulisha kichupa

11:16 AM
 
Rapa mkali wa Sinza Star Mansu-Li, anayeendeleaa kuuwakilisha muziki wa Hip Hop ambaye baada ya kutoa traki mpya ya kolabo kali na  marapa Jaymoe pamoja na The Don kupitia wimbo wao 'Leo Ndio Leo', hivi sasa anadondosha project yake mpya ambayo anatarajia kuachia kichupa kipya kwa mashabiki wake Afrika Mashariki.

HUWEZI AMINI,HUU NDIO UTAJIRI WA MAJUMBA YA KIFAHARI YA MCHEZAJI MRISHO NGASA ,JIONEE MWENYEWE HAPA

12:27 AM

SASA ni miaka nane tangu aanze kucheza soka ya 

ushindani mwaka 2005 katika klabu ya Kagera 

Sugar ya Bukoba, lakini kwa namna alivyopanga 

vyema karata zake, Mrisho Khalfan Ngasasa anafurahia

 maisha ya mpira. Huwezi kumuita tajiri, lakini huwezi 

kuacha kumpa heshima miongoni mwa wachezaji wa

 kizazi chake, kwamba amewaacha mbali. Amecheza klabu

 nne katika Ligi Kuu tu, baada ya Kagera Sugar ni Yanga 

SC mwaka 2007 hadi 2010, Azam 2010 hadi 2012 na sasa 

amerejea Jangwani.



Kwanini wanasoka wa Tanzania hawatoki kimapenzi na celebrities wa kike?

10:54 AM
20130805-141306.jpg


ZUNGUKA kumbi zote za disko. Hautamuona mwanasoka yoyote wa Tanzania amemshika kiuno mwanamke maarufu (celebrity) katika fani yoyote maarufu kuanzia, filamu, muziki hadi siasa. Na sio hao tu, wanasoka wa Tanzania wanaishi dunia tofauti na wanawake wenye hadhi za juu (high Personalities female)
Wakati David Beckham akihangaika na Victoria AdamsCristiano Ronaldo akihangaika na mwanamitindo wa Kirusi, Irina Shayk, hali ni tofauti kwa mwanasoka wa Tanzania. Ni nadra kwenda katika klabu ya usiku (Nightclub) na kumkuta Nadir Haroub ‘Cannavaro’ akiwa katika mtoko na Mwanamitindo Flavian Matata. Unajua kwa nini kuna sababu nne kubwa. Kwanza ni umaskini unaowakabili. Hawapo katika kiwango cha kushindana kifedha na mastaa wa fani nyingine ndani ya nchi. Wakati mwanamuziki Diamond anaweza kuingiza sh 30 milioni kwa shoo za mwezi mmoja, inamchukua Mrisho Ngassa miaka miwili ya kusaini mkataba mpya ndipo apate fedha hizo.
Wema Sepetu hawezi kwenda kwa Mrisho Ngassa. Atakim
 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates